» » TAKUKURU Kuwachunguza Vigogo wa Escrow kama Wameficha Pesa Nje ya Nchi


Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imesema kuwa imeamua kushirikisha taasisi zingine za kimataifa ili kuwachunguza baadhi ya watuhumiwa wa Escrow kama wamehifadhi fedha nje ya nchi.

Hayo yamesemwa na Afisa Habari na Uhusiano wa taasisi hiyo, Mussa Misalaba alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam, ambapo amesema kuwa watuhumiwa wote wa Escrow bado wanaendelea kuchunguzwa.

Amesema kuwa Takukuru inaendelea kuwachunguza watuhmiwa wote huku ikishirikiana na baadhi ya taasisi za nje na kwamba uchunguzi huo unafanyika kwa umakini zaidi ili haki itendeke.

“Hili jambo linafanyika kwa umakini mkubwa, usione kimya kuna jambo linafanyika, kwa sasa ni mapema sana kusema chochote kuhusu jambo hili kwakuwa linahitautlivu mkubwa kulishughulikia,”amesema Misalaba

Aidha, hivi karibuni TAKUKURU iliwafikisha mahakamani baadhi ya watuhumiwa wa ufisadi na uhujumu uchumi ili kujibu mashtaka yanayowakabili.

Waliofikishwa mahakamani kujibu tuhuma ni pamoja na Theofilo Bwakea, Mkurugenzi wa Kampuni ya VIP Engineering and Markerting, na aliyekuwa Mkurugenzi wa Kampuni ya IPTL, James Rugemalila wote wakikabiliwa kesi ya uhujumu uchumi

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...