» » Lowassa atiwa mbaroni Geita

EDWARD Lowassa, Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo na aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amekamatwa na Jeshi la Polisi mkoani Geita akituhumiwa kufanya mkusanyiko usio halali, anaandika Charles William.
Lowassa amekamatwa alasiri ya leo baada ya kukatiza kwa mguu katika eneo stendi ya mabasi Geita, ambapo wananchi wengi walimzunguka wakimsalimia na kusababisha msongamano mkubwa wa watu, kila mtu wakitaka kumsogelea.
Hata hivyo taarifa zaidi kutoka mkoani Geita zimeeleza kwamba, mbali na Lowassa kukamatwa lakini pia baadhi ya waandishi wa habari walipigwa na kukamatwa na askari waliofika eneo la tukio kumkamata Lowassa.
“Askari walifika wakiwa katika magari matatu huku wakiwa wamejihami kwa silaha za moto, wamewapiga waandishi wa habari na kumkamata Lowassa ambapo wamempeleka Kituo Kikuu cha Polisi Geita,” kimeeleza chanzo chetu.
Khamis Mgeja, mmoja kati ya watu waliokuwa wameambatana na Lowassa katika msafara huo amesema, Lowassa alikuwa akielekea sokoni kununua matunda na kwamba wanashangaa kwanini Polisi wamemkamata.
“Alikuwa anapita sokoni kununua matunda, watu wakajazana kumsalimia na yeye kama mtu muungwana akawa akisalimiana nao, polisi wakafika kumkamata na wamempeleka kituo kikuu cha polisi,” amesema kwa simu Mgeja alipozungumza na MwanaHALISI Online.
Taarifa zaidi kuhusu tukio hili zitakujia kwa kadri tutakavyokuwa tukipokea…

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...