» » Raila Odinga awataka wafuasi wake wagome kwenda kazini

Kiongozi wa Muungano wa Vyama vya Siasa Nchini Kenya (NASA), Raila Odinga amewashauri wafuasi wake kutoingia ofisini kuanzia leo jumatatu ili kuonyesha shinikizo la kutokubaliana na matokeo ya uchaguzi mkuu uliofanyika hivi karibuni.

Ameyasema hayo jana wakati akihutubia wafuasi wake jijini Nairobi kwa mara ya kwanza tangu kutangazwa kwa matokeo, ambapo Rais Uhuru Kenyatta alitangazwa mshindi kitu ambacho kilipingwa vikali na Odinga.

Aidha Odinga alisema kuwa siku ya Jumanne, muungano wa vyama hivyo utatoa msimamo wake kuhusu mwelekeo watakaouchukua kulingana na kutokubaliana na matokeo hayo kwa madai kuwa yamechakachuliwa.

Rais Uhuru Kenyatta alitangzwa mashindi kwa kura 8,203,290 huku Raia Odinga akipata kura 6,762,224 kitu ambacho muungano huo wa vyama vya siasa unapinga matokeo hayo kwa kusema yamebadilishwa.

Hata hivyo, Katibu mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa, Kofi Annan, ambaye alikuwa mpatanishi mkuu baada ya mzozo wa kisiasa nchini Kenya miaka kumi iliyopita, amemshauri Odinga kutumia hatua za  kisheria kutafuta haki kuhusu matokeo ya uchaguzi wa urais kama anaona kaonewa.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...