» » 30 wafariki katika mlipuko mskitini Afghanistan

mskiti Afghanistan

Haki miliki ya pichaAFP
Image captionMlipuko umesababisha uharibifu katika mskiti huko Herat
Milipuko na risasi zilizofyetuliwa katika mji uliopo Afghanistan magharibi - Herat imesababisha vifo vya watu takriban 30 na kusababisha wengine wengi kujeruhiwa.
Msemaji wa polisi katika eneo hilo amesema shambulio hilo limetekelezwa na mlipuaji wa kujitoa muhanga.
Hakuna kundi linalodai kuhusika.
Shambulio dhidi ya Mskiti wa Jawadia limetokea saa mbili usiku wakati mamia ya waumini walipokuwa wanaswali swala ya jioni.
Mskiti huo upo katika eneo la mji wa Herat ulio na idadi kubwa ya wasilamu wa madhehebu ya Shia.
Afisa wa serikali ameiambia BBC kwamba mlipuaji wa kujitoa muhanga alifyetua risasi ndani ya mskiti kabla ya kujilipua.
Herat, mji uliopo karibu na mpaka na Iran, unatazamwa kuwa mojawapo ya miji ya amani Afghanistan.
Katika mwaka uliopita, kundi la Islamic State limelenga maeneo ya Shia katika sehemu nyingi nchini.
Siku ya Jumatatu kundi hilo limekiri kuhusika na shambulio la kujitoa muhanga dhidi ya ubalozi wa Iraq katika mji mkuu Kabul.


Tuma picha/ habari what-sap 0769436440


tupe maoni yako

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn news

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...