» » Rais Magufuli amuapisha Mashiba kuwa Balozi wa Tanzania nchini Malawi

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo amemuapisha Mhe. Benedict Martin Mashiba kuwa Balozi wa Tanzania nchini Malawi

Mhe Benedict Martin Mashiba amechukua nafasi ya Mhe. Victoria Richard Mwakasege ambaye amestaafu nafasi hiyo, mbali na hilo Rais Magufuli amepokea hati za utambulisho wa Mabalozi watano walioteuliwa kuziwakilisha nchi zao hapa nchini.

Mbali na hilo Rais Magufuli amewapongeza mabalozi hao kwa kuteuliwa kuziwakilisha nchi zao hapa nchini na kuwaomba mabalozi hao kutilia mkazo diplomasia ya Uchumi kwa kuongeza juhudi za kuhamasisha wafanyabiashara na wadau wengine wa maendeleo kushirikiana na Tanzania katika biashara na miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwepo ujenzi wa viwanda, Kilimo na huduma za jamii.

Mabalozi waliowasilisha hati zao za utambulisho ni
1.Mhe. Nguyen Kim Doahn – Balozi wa Vietnam hapa nchini.

2.Mhe. Prof. Ratlan Pardede – Balozi wa Indonesia hapa nchini.

3.Mwadhama Askofu Mkuu Marek Solcynski–Balozi wa Vatican hapa nchini.

4.Mhe. Dkt. Detlef Wachter – Balozi wa Ujerumani hapa nchini.

5.Mhe. Richard Tumisiime Kabonero – Balozi wa Uganda hapa nchini.


Tuma picha/ habari what-sap 0769436440


tupe maoni yako

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn news

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...