» » Rais wa Palestina akata mawasiliano na Israel

Image captionRais Mahmoud Abbas

Rais wa Palestinian , Mahmoud Abbas amekata mawasiliano na serikali ya Israel hivyo kuzidisha mzozo ambao umekuwa ukitokota wiki nzima kuhusu hatua kali zaidi zilizochukuliwa na Israel huko mji wa kale wa Jerusalem .

Wapalestina watatu walifariki hapo jana katika makabiliano makali na maafisa wa polisi wa Israeli katika eneo hilo.

Ghasia zilizuka pale polisi wa Israeli walipoweka vizuizi kuwazuia wanaume wote chini ya miaka 50 kushiriki salah ya Ijumaa katika msikiti wa Al-Aqsa eneo linalozozaniwa na pande hizo mbili kinzani.

Eneo hilo takatifu la ibada mjini Jerusalem, maarufu kama Hara al-Sharif, kwa waumini wa kislamu na Hekalu la mlimani kwa wayahudi.

Ripoti zaongeza kusema kuwa raia watatu wa Israel pia waliuawa katika mzozo huo huko eneo la ukingo mwa magharibi - West Bank

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...