» » Uchumi wa Korea Kaskazini waimarika licha ya vikwazo

Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionUchumi wa Korea Kaskazini

Uchumi wa taifa la Korea Kaskazini uliimarika kwa haraka katika kipindi cha miaka 17 iliopita licha ya kuwekewa vikwazo kutokana na mpango wake wa kinyuklia na utengenezaji wa makombora ya masafa marefu.

Uzalishaji wa bidhaa nchini humo ulikuwa kwa asilimia 3.9 2016 ikilinganishwa na mwaka uliopita kulingana na benki ya Korea.

Ukuwaji huo unatokana na uchimbaji madini, kawi na uuzaji wa bidhaa nchini China.

Marekani imekuwa ikiitaka Beijing kukata biashara na Pyongyang huku wasiwasi ukiongezeka kuhusu mipango ya kinyuklia ya rais Kim Jong Un.

China ndio mshirika pekee mkuu wa Korea Kaskazini na mfadhili mkubwa wa misada nchini humo.

Wiki iliopita China ilitoa data ikidai kuwa Korea Kaskazini haina uwezo mkubwa kama inavyodaiwa na rais Trump.

Lakini huku Beijing ikisitisha ununuzi wa mkaa kutoka Korea Kaskazini, imeendelea kufanya biashara ya chuma na bidhaa nyengine.

Ijapokuwa Korea Kaskazini haichapishi data za kiuchumi , benki kuu ya Korea Kusini inatoa takwimu za ukuwaji kila mwaka kutokana na data yake kutoka katika wizara ya muungano na hudumu za kijasusi.

Ukuwaji mkubwa wa Korea Kaskazini 2016 ndio mkubwa zaidi tangu ukuwaji ule uliorekodiwa 1999.

Na ukuwaji wa mwaka uliopita unatokana na ule wa 2015 baada ya uchumi wa Korea Kaskazini kunyauka kwa asilimia 1.1 kufutia mporomoko wa bei za bidhaa duniani ambao uliathiri thamani ya mkaa wake na chuma.

Raia wa Korea kaskazini ni miongoni mwa watu masikini duniani huku pato la kitaifa likiwa dola 1136 kwa mwaka.

Uchumi wa Korea Kusini ni mara 20 ya mapato hayo.

Wasiwasi wa kimataifa kuhusu Korea Kaskazini uliongezeka wiki iliopita baada ya jaribio la kombora la masafa marefu , ambalo inaamini lina uwezo wa kufika Alaska nchini Marekani.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...