» » Mkwe wa Trump akana kuwasiliana na maafisa wa Urusi


Image captionMkwe wa Trump,jared Kushner akana kuwasiliana na maafisa wa Urusi

Mkwe wa rais Donald Trump Jared Kushner ataliambia jopo la seneti baadaye kwamba sio yeye wala mwanachama yeyote wa kampeni ya Trump alishirikiana na maafisa wa Urusi kuingilia uchaguzi wa Marekani.

Atasema kwamba hakuwa na mawasiliano na kwamba hakutegemea ufadhili wa Urusi kuendesha biashara zake.

Bwana Kushner alitoa hotuba yake kabla ya mkutano huo.

Bunge la Seneti ,ikulu ya Whitehouse pamoja na wakili maalum wanachunguza uingiliaji wa Urusi katika uchaguzi huo.

Bwana Kushner mwenye umri wa miaka 36 ni mshauri mwandamizi wa rais na alikuwa akisimamia kampeni ya Trump kuhusu maswala ya mipango ya kidijitali.

Amemuoa mwana wa Trump Ivanka.

Mkwewe Trump aizuru Iraq rasmiFBI wamchunguza mkwe wa Trump, KushnerTrump amtetea mkwe wake kuhusu Urusi

Kushner ambaye hufanya mambo yake kwa usiri mkubwa atahudhuria kikao cha kamati ya upepelzi katika bunge la seneti kabla ya kuwasili mbele ya bunge la Congress siku ya Jumanne.

Katika taarifa hiyo aliyotoa siku ya Jumatatu, anasema: Sikushirikiana wala sijui mtu yeyote aliyejihusisha na serikali yoyote ya kigeni.

Image captionJared Kushner na Ivanka Trump

''Kuhusu mawasiliano na Urusi ama mwakilishi wa Urusi wakati wa kampeni'' ,hakuna alisema.

Mwisho wa taarifa hiyo anazungumzia kuhusu kumiliki anwani za watu wanne wanaowakilisha Urusi wote ikiwa wakati wa kampeni na baadaye.

Alikuwa akizungumzia mkutano na wakili wa Urusi Natalia Veselnitskaya mnamo mwezi Juni mwaka uliopita.

Wakili huyo alikuwa amemuahidi habari ambayo ingemuharibia jina Hillary Clinton.

Bwana Kushner alisema kuwa aliwasili kuchelewa katika mkutano huo na akagundua kwamba kulikuwa hakuna cha mno kilichokuwa kikizungumziwa.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...