» » Marekani na China zakosa kuafikiana kibiashara


Image captionMeli ya mizigo ya China

Marekani na China zimekamilisha mkutano wa kibiashara kuhusu maswala tata mjini Washington bila maafikiano.

Pande zote mbili hazikutoa taarifa ya pamoja ama hata mpango baada ya mkutano huo na kufutilia mbali mikutano na vyombo vya habari iliotarajiwa kufanyika.

Marekani ilikosoa biashara ya China na kutaka makubaliano ya kibiashara ambayo hayatapendelea upande mmoja.

Rais Donald Trump amesema kuwa ushuru kuhusu vyuma vya China bado huenda ukatekelezwa.

Katika hotuba yake ya ufunguzi wa mkutano huo wa kibiashara kati ya mataifa ya China na Marekani, katibu wa biashara nchini Marekani Wilbur Ross aliikosoa biashara ya ziada ya China yenye thamani ya dola bilioni 347 akisema kuwa haitokani na mvutano wa kisoko.

Katika taarifa fupi, bi Ross na katibu katika wizara ya fedha Steven Mnuchin alitoa maelezo machache na ishara kuhusu hatua zilizopigwa kuhusu maswala tata.

''China ilitambua kwamba pendekezo letu la kupunguza tofauti ya kibiashara kati ya pande zote mbili litaafikiwa'', taarifa hiyo ilisema.

Swala tata la kodi itakayotozwa vyuma vya China lilitarajiwa kuwa mjadala mgumu katika mkutano huo, lakini pande zote mbili hazikutoa taarifa yoyote.

Marekani inalaumu biashara ya ziada ya vyuma vya China ambayo inaathiri wazalishaji wa Marekani na sasa imeonya kuweka kodi.

Kampuni za kuuza vyuma nchini Marekani hazikufanya biashara nzuri huku wawekezaji wakidhani kwamba Marekani huenda ikaitoza kodi China kwa biashara ya ziada ya vyuma vyao vinavyoingia Marekani.

Baada ya soko kufungwa, rais Trump aliwaambia maripota kwamba kodi ya vyuma inaweza kutekelezwa kulingana na chombo cha habari cha Reuters.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...