» » ADC Nao Wampinga Tundu Lissu

Chama cha Alliance For Democratic Change (ADC) wameitaka Chadema itoe msimamo wake kuhusu kauli ya mwanasheria wa chama hicho, Tundu Lissu kutaka jumuiya za kimataifa zisitishe misaada kwa Tanzania.

Katibu Mkuu wa ADC, Doyo Hassan amesema kama huo hautakuwa msimamo wa Chadema ,Lissu anapaswa kuomba radhi.

Amesema kauli ya kutaka misaada isitishwe hailengi kuwatakia mema Watanzania.

"Tunadhani matatizo yetu ya ndani ni vema tukapambana nayo kuliko kutangazia ugomvi wako kwa mtu asiyekuhusu.’’

"Kwa kauli hii hizi za Chadema ni wazi wameshindwa mapambano ya ndani na sasa wanafikiria njia nyingine ambazo ni hatari zaidi katika nchi yetu,"amesema Hassan.

Amesema kama Chadema imeshindwa kupambana na CCM na Serikali yake ni wazi wawaeleze wafuasi wao kuliko kutoa matamshi ambayo yanahatarisha ustawi wa taifa letu.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...