Image captionWapiganaji wa Boko haram
Kampuni ya mafuta ya Nigeria N-N-P-C, inasema kuwa watafiti 10 wa jiologia, wametekwa nyara na washukiwa wa kundi la Boko Haram
Wanajiolojia hao na masoroveya wa Chuo Kikuu cha Maiduguri, waliviziwa na kutekwa nyara karibu na kijiji cha Jibi kilichoko katika jimbo la Borno, Kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.
Walikuwa wamepewa kandarasi ya kutafuta mafuta karibu na ziwa Chad.
Taarifa nyingine kutoka maeneo hayo, inasema kuwa kuna hofu wameuawa, lakini hilo halijathibitishwa.

No comments:
Post a Comment