» » Afrika Kusini kujitoa ICC?


Haki miliki ya pichaAPImage captionRais Omar al Bashir amekuwa kiongozi wa Sudan tangu mapinduzi ya mwaka 1989

Chama tawala nchini Afrika kusini kimeonesha kuwa bado kina mipango ya kuiondoa Afrika kusini kwenye uanachama na Mahakama ya kimataifa ya uhalifu, ICC.

ICC inatarajia kutangaza siku ya alhamisi kama Afrika Kusini ilivunja sheria kwa kushindwa kumkamata Rais wa Sudan Omar al Bashir, alipoitembelea nchi hiyo mwaka 2015.

Rais Bashir anashutumiwa kutekeleza mauaji ya kimbari wakati wa mzozo wa Darfur.

Serikali ya Afrika kusini ilikua na mipango hiyo tangu miaka miwili iliyopita.

Ilikua ni msukumo uliofanywa na baadhi ya serikali za Afrika dhidi ya taasisi hiyo zikidai kuwa ICC imekua ikilionea bara la Afrika na viongozi wake.

Mahakama kuu nchini Afrika Kusini yenyewe imesema serikali imekua ikifanya mchakato huo kinyume na katiba, ikishindwa kulipeleka suala hilo bungeni.

Pamoja na hayo chama cha ANC kimesema hakitarudu nyuma, wataendelea na mipango yao ya kujiondoa ICC.

Download Apps Yetu Gsn News
Au tupigie kwa 0769436440

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...