» » Rais Magufuli Atoa Neno Kwa Watumishi wa Uma

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Magufuli leo wakati akizindua Mfumo wa serikali wa ukusanyaji kodi kwa njia ya Kieletroniki amewachana baadhi ya watumishi wake akisema wamekuwa wakiwaza mambo makubwa ambayo wanashindwa hata kuyatimiza.

Rais Magufuli amesema kuwa watumishi wengi wamekuwa si wabunifu katika kuangalia vyazo vya mapato ambavyo vinaweza kusaidia serikali kuingiza pesa nyingi lakini wao wamekuwa wakiwaza kuongeza bei ya pombe tu na kuacha vitu vingine ambavyo vingeweza kuongeza mapato kwa serikali kwa njia nyingine nzuri.

"Saizi watu wanahangaika na Machinga wakati tungeweza kutengeneza vitambulisho vya wamachinga na kila kimoja tukauza labda elfu kumi, Machinga akinunua kitambulisho hicho anatambulika na serikali na kinaeleza kuwa anapaswa kuwa wapi, je, ni shilingi ngapi tungezipata hapo kwa idadi wa wamachinga waliopo nchi nzima? Lakini watu wetu wao wanawaza kuongeza bei ya pombe tu, yaani tuna watu wa uchumi wengi lakini sijui hata wanafikiria nini " alisema Rais Magufuli

Mbali na hilo Rais Magufuli alisema hata tabia ya watu kukwepa kulipa kodi inasababishwa na mipango mibovu akitolea mfano kuwekwa bei juu ya kodi ya majengo jambo ambalo linafanya watu wengine kushindwa kulipa kodi hiyo na serikali kupoteza mapato.

"Watu wetu hawa hata kwenye kodi ya majengo unakuta wameweka mtu alipe milioni mbili sasa hizo pesa wananchi wanazipata wapi? Ndiyo maana wanakwepa kodi sababu hawana pesa hizo lakini kama wangeweka labda elfu kumi, ishirini mpaka hamsini halafu wenye maghorofa labda laki mbili ungeona kila mtu angekimbilia yeye mwenyewe kulipa kodi, kwa nyumba zote zilizopo Tanzania tungepata shilingi ngapi? Lakini wameweka pesa kubwa na hawazipati sababu watu hawalipi hawana hizo pesa" alisisitiza Rais Magufuli

Katika hatua ya mwisho Rais Magufuli aliyaomba makampuni ya simu nchini yawe mfano wa kuingwa na ikiwezekana yawe ya kwanza kabisa kujiunga katika mfumo huu mpya wa ukusanyaji wa kodi kwa njia ya kieletroniki kwani mfumo huu una manufaa kwa wawekezaji na Watanzania kwa ujumla.



Tuma picha/ habari what-sap 0769436440

BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS

tupe maoni yako

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...