Rais wa Syria, Bashar al-Assad, amefanya ziara ya ghafla isiyotarajiwa nje ya mji mkuu wa nchi hiyo Damascus, alikohudhuria maombi ya Eid, katika mji wa Hama, zaidi ya kilomita 200 kaskazini mwa nchi hiyo.
Ni sehemu ya mbali zaidi kuwahi kusafiri, ndani ya Syria, tangu mapigano yalipoanza nchini humo miaka 6 iliyopita.
- Urusi yatakiwa kuacha kumuunga mkono Bashar al-Assad
- Trump: Bashar Al Assad ni mtu katili
- Bashar al-Assad: Syria kushirikiana na Marekani
- Assad asema ushindi Aleppo ni muhimu
Runinga ya nchi hiyo, ilipeperusha picha ya Rais Assad, akisali ndani ya msikiti mmoja mkubwa mjini Hama nyumba ya imamu wa msikiti huo, ndani ya umati mkubwa wa waumini wengine.
Ziara hiyo ya Assad inatukia wakati ambapo wanajeshi wa serikali yake, wakiungwa mkono na ndege za kijeshi za Urusi, wakiendelea kupata nguvu dhidi ya makundi ya waasi.
Tuma picha/ habari what-sap 0769436440
BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI