Haki miliki ya pichaAFP/GETTY IMAGESImage captionMsako na shughuli za uokozi zinaendelea
Idara ya polisi nchini Colombia, imesema kuwa yamkini watu 6 wamefariki ika ajali ya kuzama kwa boti moja la abiria katika bwawa moja, katika mji mmoja ulioko kaskazini magharibi mwa nchi hiyo.
Watu 16 hawajulikani waliko, baada chombo cha ghorofa nne, lilipoanza kujaa maji mara tu lilipo n`goa nanga katika ziwa moja la kujiundia, karibu na mkahawa mmoja maarufu kwa watalii la Guatapé, kilomita 45 mashariki mwa Medelini, siku ya Jumapili.
Hakujatolewa taarifa zaidi ya kilichosababisha chombo hicho cha majini kuzama.
"Hali inaonekana kuwa mbaya zaidi," afisa mmoja wa serikali katika eneo hilo amewaambia wanahabari.
Zaidi ya watu 20 wamekimbizwa hospitalini katika mji wa Guatapé.
Image captionRamani inayoonyesha mji wa Guatape
Luis Bernardo Morales, kapteni mmoja wa idara ya zima moto ambaye anahusika moja kwa moja katika shughuli za uokoaji, amesema kuwa boti hilo lilikuwa karibu na bandari pale lilipozama.
"Hatujafahamu kama kiini cha ajali hiyo ilikuwa ni matatizo ya kimitambo, ubeba watu kupita kiasi au mawimbi ziwani," Shirika la habari la AFP lilimnukuu akisema.
Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.