headlines

    07:4
» » Mashua yazama Colombia 6 wafa maji, 16 hawajulikani waliko

Msako na shughuli za uokozi zinaendelea

Haki miliki ya pichaAFP/GETTY IMAGES
Image captionMsako na shughuli za uokozi zinaendelea
Idara ya polisi nchini Colombia, imesema kuwa yamkini watu 6 wamefariki ika ajali ya kuzama kwa boti moja la abiria katika bwawa moja, katika mji mmoja ulioko kaskazini magharibi mwa nchi hiyo.
Watu 16 hawajulikani waliko, baada chombo cha ghorofa nne, lilipoanza kujaa maji mara tu lilipo n`goa nanga katika ziwa moja la kujiundia, karibu na mkahawa mmoja maarufu kwa watalii la Guatapé, kilomita 45 mashariki mwa Medelini, siku ya Jumapili.
Kulikuwa na watu 150 ndani ya chombo hicho.
Kwa mjibu wa mtu mmoja aliyeshuhudia ajali hiyo, Juan Quiroz, ameiambia BBC kuwa, chombo hicho kilichukua chini ya dakika 5 kuzama.
Image captionWalio okolewa wam,etamaushwa na ajali hiyo
Maboti mengine madogo madogo yalifika kwa kasi na kuanza kuwaokoa watu kutoka majini na orofa ya juu ya chombo hicho.
Aidha, ndege za helikopta na wapiga mbizi wa kijeshi wameonekana mahali pa mkasa huo wakijaribu kuwaokoa manusura.
Hakujatolewa taarifa zaidi ya kilichosababisha chombo hicho cha majini kuzama.
"Hali inaonekana kuwa mbaya zaidi," afisa mmoja wa serikali katika eneo hilo amewaambia wanahabari.
Zaidi ya watu 20 wamekimbizwa hospitalini katika mji wa Guatapé.
Image captionRamani inayoonyesha mji wa Guatape
Luis Bernardo Morales, kapteni mmoja wa idara ya zima moto ambaye anahusika moja kwa moja katika shughuli za uokoaji, amesema kuwa boti hilo lilikuwa karibu na bandari pale lilipozama.
"Hatujafahamu kama kiini cha ajali hiyo ilikuwa ni matatizo ya kimitambo, ubeba watu kupita kiasi au mawimbi ziwani," Shirika la habari la AFP lilimnukuu akisema.
Guatapé ni eneo maarufu kwa watalii katika mji wa Andean, unaojulikana kwa michezo mingi ya majini na sehemu ya burudani.


Tuma picha/ habari what-sap 0769436440


BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS


tupe maoni yako

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...