headlines

    07:42 A
» » Jeshi la Polisi latoa tahadhari kwa watumiaji wa barabara


Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani limetoa tahadhari kwa watumiaji wote wa barabara nchini kuzingatia sheria ili kuepuka ajali hususani wakati wa sikukuu ya Eid el Fitri.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam jana juni 25, 2017, Kaimu Kamanda Kikosi cha Usalama Barabarani, (SACP) Fortunatus Musilimu alisema kuwa katika kipindi cha sikukuu madereva wamekuwa wakiendesha magari kwa mwendo kasi, kuyapita magari mengine bila kuchukua tahadhari na kubeba abiria kupita kiasi hali inayoweza kusababisha ajali.

“Tutafanya operesheni kali barabarani, kuwapima madereva kiwango cha ulevi na watakaobainika wamelewa watakamatwa na kuwekwa mahabusu na kufikishwa mahakamani, nasisitiza kwamba,dereva anayetaka kuendesha gari asinywe pombe,akitaka kunywa pombe asiendeshe gari” alisisitiza Kamishna Musilimu katika taarifa hiyo.

Wamiliki wa magari wametahadharishwa yatakayokodishwa  kwenda maeneo ya Fukwe bila kibali yatakamatwa na wahusika kufikishwa mahakamani.

Kamishna Musilimu pia alitoa wito kwa wazazi kuangalia usalama wa watoto wao na wasiwaache wakatembea peke yao barabarani bila uangalizi ili kuepuka ajali zinazoweza kuepukika.

Akizungumzia upande wa madereva wa Pikipiki (Bodaboda) alieleza kuwa wamekuwa wakipita taa nyekundu, wakiendesha pikipiki zao bila kuvaa kofia ngumu, kubeba abiria zaidi ya mmoja (mishikaki) na abiria hao kutovaa kofia ngumu hivyo kuhatarisha Usalama wao hivyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Kamishna Musilimu alisema, Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani limekuwa likihamasisha na kuelimisha wananchi kuhusu umuhimu wa kuzingatia sheria na matumizi sahihi ya barabara ili kuepuka ajali katika kipindi chote na hasa wakati huu wa sikukuu.


Tuma picha/ habari what-sap 0769436440


BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS



tupe maoni yako

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Mashua yazama Colombia 6 wafa maji, 16 hawajulikani waliko
»
Previous
Magazeti ya Leo Jumatatu ya June 26

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...