» » Korea Kaskazini yafanyia majaribio mashine zake

Korea Kaskazini yafanyia majaribio mashine zake

Image captionKorea Kaskazini yafanyia majaribio mashine zake
Maafisa wa Marekani wanaamini kwamba Korea kaskazini ilitekeleza jaribio jingine la mashine ya kurushia makombora yake .
Jaribio hilo linadaiwa kutekelezwa siku ya Jumatano litakuwa jaribio la kwanza la mashine kama hiyo kutekelezwa na Korea Kaskazini tangu mwezi Machi.
Habari hiyo inajiri wakati ambapo kuna wasiwasi kati ya washington na Pyongyang kuhusu mpango wa kinyuklia wa Korea kaskazini.
Utawala wa Trump umefanya swala hilo kuwa swala kuu.
Licha ya shutuma za kimataifa ,Korea Kaskazini imeongeza majaribio yake ya makombora kwa lengo la kutengeza kombora linaloweza kurushwa kutoka bara moja hadi jingine.
Shirika la ujasusi la Marekani limeonya mwezi uliopita kwamba Korea Kaskazini linakaribia kufanikiwa katika mpango huo.
Maafisa wa Marekani waliokuwa wakizungumza kwa vitengo kadhaa vya habari walisema hatua hiyo ya hivi karibuni siku ya Alhamisi ni awamu ya kwanza ya kutengeza kombora la masafa marefu ambalo litaweza kufika Marekani.
Kutokana na kiwango cha siri cha vitendo vya majeshi yote ya Korea Kaskazini, ni vigumu kwa wataalam kuangazia hatua ilizipogwa na taifa hilo kutengeza kombora la masafa marefu.
Rais wa Korea Kaskazini Kim Jong Un
Image captionRais wa Korea Kaskazini Kim Jong Un
Mashine hizo zinaweza kutumika katika kurusha satelaiti angani, lakini maafisa wa Marekani wana wasiwasi teknolojia hiyo inajaribiwa kutengeza kombora linaloweza kurushwa kutoka bara moja hadi jingine.


Tuma picha/ habari what-sap 0769436440


tupe maoni yako

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn news

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...