» » Mwandani wa aliyekuwa rais wa K. Kusini afungwa jela

Mwandani wa aliyekuwa rais wa K. Kusini Park Geun Hye ,Choi Soon-sil afungwa jela

Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionMwandani wa aliyekuwa rais wa K. Kusini Park Geun Hye ,Choi Soon-sil afungwa jela
Mwandani wa aliyekuwa rais wa Korea Kusini amehukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela baada ya kupatikana na hatia ya kufanya ufisadi.
Kushtakiwa kwa Choi Soon-sil ambako ni kwa kwanza baada ya kuomba zabuni kwa niaba ya mwanawe ni miongoni mwa kashfa zilizosababisha kuangushwa kwa utawala wa rais Park Geun hye.
Alifanya kazi kwa miaka minne kama mshauri wa bi Park ambaye alihojiwa na baadaye kushtakiwa.
Choi pia anakabiliwa na mashtaka kwamba alikubali hongo kutoka kwa Park.
Bi Park amekana madai yote ya ufisadi.
Choi alipatikana na hatia ya kutumia wadhfa wake kushawishi maafisa wa chuo kikuu kumuingiza katika shule hiyo mwanawe wa kike, mbali na kumpatia alama za mitihani ambayo hakufanya.
Mahakama ilisema katika uamuzi wake kwamba alifanya makosa mengi kuonyesha kuwa vitendo vyake vilikuwa upendo wa mama ambaye alitaka mwanawe kufanikiwa kulingana na chombo cha habari cha Yonhap.
Maafisa wawili wa zamani katika chuo kikuu cha Ewha Womens University mjini Seoul pia wamefungwa kwa kushirikiana na Choi.
Choi pia anakabiliwa mashtaka mengine ikiwemo kutumia vibaya mamlaka, kulazimisha, kujaribu kulazimisha na kujaribu kufanya udanganyifu.
Waendesha mashtaka wanasema mwanawe bi Chung alihusika na uhalifu wa kiuchumi, udanganyifu katika mitihani, kuzuia biashara na kuficha kesi ya jinai.


Tuma picha/ habari what-sap 0769436440


tupe maoni yako

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn news

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...