» » Trump akana kumrekodi aliyekuwa mkurugenzi wa FBI

Donald Trump na aliyekuwa mkurugenzi wa shirika la ujasusi nchini Marekani FBI James Comey

Image captionDonald Trump na aliyekuwa mkurugenzi wa shirika la ujasusi nchini Marekani FBI James Comey
Rais wa Marekani Donald Trump amesema kuwa hakumrekodi aliyekuwa mkurugenzi mkuu wa shirika la FBI James Comey licha ya kudai hivyo hapo awali.
Alituma ujumbe katika mtandao wake wa Twitter kwamba hakutengeza na wala hana rekodi hizo siku moja baada ya kutakiwa kuwasilisha kanda hizo kwa jopo la Congress.
Bwana Trump alianzisha uvumi wa rekodi hizo katika ujumbe wa Twitter aliochapisha siku moja baada ya kumfuta kazi bwana Comey mnamo mwezi Mei.
Alisema: James Comey uwe na matumaini kwamba sina sina rekodi zozote za sauti yako kuhusu mazungumzo yetu.
Chapisho hilo lilizua madai chungu nzima kwamba bwana Comey alifutwa kazi ili kuzuia uchunguzi kuhusu Urusi kuingilia Uchaguzi wa Marekani mwaka uliopita mbali na ushirikiano wake na kampeni ya rais Donald Trump mjini Moscow.
Licha ya lengo lake kutobainika, ujumbe huo wa Twitter ulisababisha kuajiriwa kwa mtaalam ambaye amechukua uongozi wa uchunguzi wa madai hayo.
Swala hilo linatokana na uchaguzi wa urais wa mwaka jana na ushahidi unaotolewa kwamba wadukuzi wa Urusi walilenga mifumo ya uchaguzi ya Marekani kwa lengo la kumsaidia Donald Trump kushinda kitu ambacho Moscow inakana.

Tuma picha/ habari what-sap 0769436440


tupe maoni yako

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn news

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...