» » Mpango wa afya, Obamacare wafikia tamati: Trump

Trump
Image captionUtawala wa Rais Donald Trump umekuwa ukishangilia
Utawala wa Rais Donald Trump umekuwa ukishangilia baada ya Bunge la wawakilishi kupitisha muswada uliobatilisha mpango wa afya wa Obamacare ,sheria ya Obama kuhusu gharama nafuu za upatikanaji wa matibabu.
Mpango huo wa huduma za afya wa Obama ulikuwa ukitoa huduma za bima ya afya kwa mamilioni ya raia wa Marekani, hivyo kutengua mpango huo ulikua moja ya ahadi ya Trump wakati wa Kampeni za urais.
Muswada huo umepita kwa ushindi mwembamba wa kura 217 kwa 213.
Muswada huo sasa utapelekwa kwenye bunge la Senate ambao walitoa wito wa kufanyika kwa mabadiliko ya sheria.
Mwandishi wa BBC mjini Washington amesema muswada huo haujulikani utaathiri watu wangapi kutokana na kupoteza bima za afya.
TrumpHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionRais Trump ameseama ana uhakika muswada huo utapita kwenye bunge la Senate
Akizungumza baada ya kupigwa kura, rais Trump ameseama ana uhakika muswada huo utapita kwenye bunge la Senate.
'' kwa miaka miwili nimekuwa nikifanya kampeni na nawaambia kila nilipokuwa nikienda, watu walikuwa wakiathiriaka na mpango huu wa Obamacare, kwa kuwa mimi ninahusika kwenye hili nataka kuwambia kuwa gharama za matibabu zitaanza kushuka, tutahakikisha muswada huu unapita kwenye bunge la senate, nina uhakika''
upande wa wawakilishi kutoka chama cha Democrat wameeleza madhara ya kura hii iliyopigwa, Steny Hoyer ni mwakilishi ndani ya bunge upande wa walio wachache
''wabunge wengi ndani ya bunge la uwakilishi walijua wanaupigia kura muswada mbaya hii leo na Marekani yapaswa kusikitika kwa sababu wabunge wote hawakupiga kura kuipinga, na Marekani itawawajibisha''
baada ya kura hiyo waandamanaji walikua wakiimba kuonyesha kutounga mkono kura hiyo iliyopitisha muswada huo


Tuma picha/ habari what-sap 0769436440

BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS

tupe maoni yako

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...