» » Wateja wa Facebook wakaribia bilioni 2

Mtandao wa facebook wakaribia kufikisha wateja bilioni 2

Image captionMtandao wa facebook wakaribia kufikisha wateja bilioni 2
Faida ya mtandao wa facebook imepanda katika kipindi cha miezi mitatu ya mwaka huku mtandao huo ukikaribia kupata wateja bilioni 2 kulingana na ripoti ya matokeo ya mtandao huo.
Idadi ya watu wanaotumia mtandao huo kila mwezi iliongezeka hadi bilioni 1.94, ambao watu bilioni 1.3 huutumia kila siku kulingana na kampuni hiyo.
Kampuni hiyo ya Kiteknolojia nchini Marekani iliripoti faida za takriban dola bilioni 3 katika robo ya kwanza ya mwaka ambayo ni ongezeko la asilimia 76 kwa mwaka.
Hatahivyo imeonya kwamba ukuwaji wa mapato ya matangazo huenda ukashuka.
Kampuni hiyo pia imepata shinikizo kubwa katika majuma ya hivi karibuni kuhusu vile ambavyo imekuwa ikiangazia maswala ya matamshi ya chuki na unyanyasaji wa watoto.
Siku ya Jumatano ,Mkurugenzi mkuu wa kampuni hiyo Mark Zuckerberg alitangaza kwamba atawaajiri watu 3000 zaidi kuweka maudhui ya wastani katika mtandao huo.
Robo ya idadi ya watu duniani inatumia facebook kila mwezi huku watumiaji wapya wakitoka nje ya bara Ulaya na Marekani Kaskazini.
Akizungumza baada ya ripoti hiyo ya matokeo ,bwana Zuckerberg alisema kwamba idadi ya watumiaji wake wameipatia Facebook fursa ya kupanua jukumu la mtandao huo ,kuanzisha runinga, afya na siasa.


Tuma picha/ habari what-sap 0769436440


BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS



tupe maoni yako

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...