» » Aliyekuwa rais wa Korea Kusini afikishwa mahakamani kuanza kesi


Haki miliki ya pichaREUTERSImage captionBi Park alifikishwa mahakamani akiwa amefungwa pingu

Rais wa zamani wa Korea Kusini, Park Geun-Hye amefikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza mjini Seoul kwa tuhuma za ufisadi.

Hii ndio mara ya kwanza ameonekana hadharani tangu kuondolewa madarakani na kuzuiliwa mwezi Machi mwaka huu. Amekanusha kufanya makosa yeyote.

Rais wa zamani wa Korea Kusini ashtakiwaRais wa zamani Korea Kusini akamatwa

Bi Park alifika mahakamani akiandamana na rafiki wake wa karibu, Choi Soon-Sil ambae anatuhumiwa kwa kujipatia fedha kutoka kwa makampuni makubwa.

Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionBi Park Geun-hye (kushoto)na Choi Soon-sil (kuliat) wakiwa mahakamani

Alipofika mahakamani Park Guen-Hye aliulizwa ajira yake na kujibu hana hajaajiriwa.

Yeye na rafiki wake huyo hawakuzungumziana na walikaa kando ya mawakili wao. Rais huyo wa zamani alivalia mavazi meusi na siyo sare za wafungwa ambazo amekua akivalia gerezani.

Feri iliyozama Korea Kusini miaka 3 iliyopita yainuliwa

Alikua pia na kibandiko cha nambari yake ya mfungwa 503. Nywele zake zilifungwa kwa kipini kilichotolewa na mamlaka za gereza. Kwa sasa kiongozi huyo anakumbwa na njiya panda baada ya kuondolewa kwenye ikulu.

Haki miliki ya pichaEPAImage captionChoi Soon-sil alifikishwa mahakamani mapema mwaka huu

Mshirikishe mwenzako 

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...