Wakenya watawala mbio za London Marathon
REUTERS
Wakenya Mary Keitany na Daniel Wanjiru wameibuka washindi wa mbio za London Marathon.
Keitany ameandikisha rekodi mpya ya wanawake pekee katika mbio za nyika kwa muda wa 2:17:01.
Amechukua taji hilo kwa mara ya tatu sasa akiwa na miaka 35.
Muithiopia Tirunesh Diababa amemaliza katika nafasi ya pili kwa muda wa 2:17:56
Katika mbio za wanaume Daniel Wajiru wa Kenya ameshinda kwa muda wa 2:05:56 na kufuatwa kwa karibu na Kenenisa Bekele wa Ethiopia

Tuma picha/ habari what-sap 0769436440
BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS
tupe maoni yako
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

No comments:
Post a Comment