Msichana wa miaka 8 aeleza alivyonusurika ajali ya kuzama kwa gari
FACEBOOK
Msichana wa umri wa miaka 8 ambaye alinusurika wakati gari alimokuwa lilizama na kuwaua watu watatu wa familia ameelezea alivyojikakamua kujiokoa.
Chloe Kabealo anasema alifungua mshibi na akajaribu kupanda kupata hewa ndipo akapata fursa ya kuelea.
Chloe mama yake ,dada yaka na nduguye walikuwa ndani ya gari katika mjio wa Tumbulguni wakati liliteleza na kutumbukia kwenye mto uliokuwa na maji mengi mapema mwezi huu.
Chloe alifanikiwa kujiokoa na kukimbia kwa nyumba moja kutoa habari
- Timu ya Urusi ya sarakasi yapata pigo
- Waliowaua raia 10 wa Ethiopia washtakiwa
- Gari la Uber linalojiendesha lahusika katika ajali Marekani
- Uber yaondoa magari yanayojiendesha barabarani
Mama yao Stephanie King mwenye umri wa maiak 43, alikufa wakati akijaribu kuwaokoa watoto wake.
Mwanamke huyo alipatikna akiwa amefariki huku akimshika mtoto wake ishara kuwa alijaribu kuwaokoa watoto kabla hajafariki.
Ella Jane, mwenye umri wa miaka 11, na Jacob mwenye uri wa miaka 7 walifariki.
Tuma picha/ habari what-sap 0769436440
BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

No comments:
Post a Comment