Huyu ndie Mwandishi maarufu Kuki Gallmann apigwa risasi na kujeruhiwa Kenya
AFP
Watu waliojihami na bunduki wamempiga risasi na kumjeruhi mwanamazingira na mwandishi mzoefu mzaliwa wa Italia, Kuki Gallmann.
Amepigwa risasi ya tumbo akiwa kwenye shamba lake kaunti ya Laikipia.
Mwezi uliopita makahawa wake wa kifahari uliteketezwa na watu wanaoshukiwa kuwa wafugaji.
Bi Gallmann, amekuwa mwenyeji wa Kenya tangu miaka ya sabini, na anafahamika zaidi kutokana na kitabu chake 'I Dreamed of Africa'.
Filamu ya kitabu hicho pia ilitolewa, mhusika mkuu, akiwa mwigizaji maarufu wa Marekani , Kim Basinger.
THE STAR, KENYA
Tuma picha/ habari what-sap 0769436440
BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

No comments:
Post a Comment