Korea Kaskazini yasema itazamisha meli ya Marekani
AFP
Korea Kaskazini iko tayari kuzamisha meli ya kubeba ndege ya Marekani inayoelekea rasi ya Korea, kwa mjibu wa vyombo vya habari vya Korea Kaskazini.
Taarifa katika gazeti la Rodong Sinmun lilisema kuwa meli ya Marekani ya USS Carl Vinson itazamishw kwa shambulizi moja.
Kundi la meli za Marekani zikiongozwa na Vinson zinatarajiwa kuwasili katika rasi ya Korea wiki hii.
- Marekani yapeleka meli za kivita katika rasi ya Korea
- Trump aionya tena Korea Kaskazini
- Marekani yatishia kuiadhibu Korea Kaskazini
- Marekani: Hatutaivumilia tena Korea Kaskazini
- Nani alimrukia Kim Jong-un?
Meli hizo zilitumwa na Rais Donald Trump baada ya onyo kuhusu uvumilivu kumalizika dhidi ya mpamgo ya nuklia ya Korea Kasakazini.
"Vikosi vyetu viko tayari kuzamisha meli hiyo ya kubeba ndege ya Marekani kwa shambulizi moja, lilisema gazeti la Rodong Sinmum.

Tuma picha/ habari what-sap 0769436440
BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

No comments:
Post a Comment