Wanamgambo elfu mbili wa IS wauawa Iraq tokea Februari
Hivi ni viunganisho vya nje na vitafungua katika dirisha mpyaSambaza habari hii Facebook Sambaza habari hii Twitter Sambaza habari hii Messenger Sambaza habari hii Email Mshirikishe mwenzako
Image captionIS bado ni tishio nchini Iraq
Jeshi la Marekani limesema linaamini kuwa takriban wanamgambo elfu moja wa Islamic State wameuawa tokea kuanza kwa oparesheni ya kuwaondoa Magharibi mwa mji wa Iraq, Mosul.
Msemaji wa jeshi la Marekani linalounga mkono jeshi la Iraq, amesema kuwa walikuwepo wanamgambo takriban elfu mbili mwezi Februari.
Na kwa sasa wanaamini wamesalia pungufu ya nusu ya hao.
Pamekuwa na wiki ya mapigano makali mjini Mosul.
Sambamba na kuuawa kwa wanajeshi kutoka kila pande, pamekuwepo pia na taarifa za kuuawa kwa wananchi wengi.
Mshirikishe mwenzako

No comments:
Post a Comment