» » » UN yalaani mauaji ya watoa misaada Sudan Kusini

UN yalaani mauaji ya watoa misaada Sudan Kusini

Umoja wa mataifa umelaani vikali mauaji ya wafanyakazi sita wa kutoa misaada nchini Sudan Kusini.
Miongoni mwa waliouawa ni raia watatu kutoka Kenya, na watatu kutoka Sudan Kusini ambao walitekwa siku ya Jumamosi walipokuwa wakisafiri kutoka mji mkuu Juba kwenda mji wa Pibor.
Hili ni tukio la tatu la aina hiyo ndani ya mwezi mmoja likiwa limepoteza maisha ya watu wengi tokea kuanza kwa mgogoro huo mwaka 2013.
Mkuu wa mashirika ya kibinaadam nchini Sudan Kusini Eugene Owusu ameelezea mauaji hayo kama uhalifu wa kutisha.

Wafanyakazi 12 wa mashirika ya kutoa misaada waneuawa mwaka huu, wakati huu ambapo wanajaribu kuelekea sehemu ambazo umaskini ni mkubwa kutokana na vita.

http://www.bbc.com/swahili

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About IVST TANZANIA

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles