» » » Hong Kong yamchagua kiongozi mpya wa kwanza mwanamke

Hong Kong yamchagua kiongozi mpya wa kwanza mwanamke

· 
Carrie Lam amechaguliwa kuwa kiongozi mpya wa Hong Kong, akiwa ndiye mwanamke wa kwanza kushika wadhifa huo.
Bi Lam mwenye umri wa miaka 59 aliungwa mkono na serikali ya China na alitarajiwa sana kushinda,
Hong Kong ina uhuru kutoka China lakini maandano yamekuwa yakiongezeka kupinga uingiliajia wa China.
Kiongozi wa Hong Kong hachaguliwi na wananchi bali kamati ya watu 1200 iliyo na watu wengi wanaoipendelea China.
Makundi ya kupigania demokrasia yamekuwa yakifanya maandamano nje ya eno kulikofanyika uchaguzi huo na kuutaja kuwa usio wa haki.
Haki miliki ya pichaEPAImage captionCarrie Lam akishangilia ushindi
Mshindani mkuu wa Bi Lam ambaye ni mkuu wa zamani wa masuala ya uchumi John Tsang, alikuwa akipendelewa na watu kwa mujibu wa kura ya maoni.
Mgombea wa tatu alikuwa ni jaji mstaafu Woo Kwok-hing.
Bi Lam alipata kura 777 huku Tsang akipata kura 365 na Woo kura 21.
Wito wa kufanyika kwa uchaguzi huru umeshindwa licha ya kushuhudiwa maandamano makubwa.

Kamati ya uchaguzi mjini Hong Kong ilimchagua Bi Lam kuchukua mahala pa kiongozi wa sasa CY Leung, ambaye ataondoka madarakani mwezi Julai.

http://www.bbc.com/swahili

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...