Hatma ya Joe Hart kusubiri Manchester City
- posted about 1h ago
- 1-03-2017 9:56
- Michezo
Mlinda lango namba moja wa timu ya Taifa ya Uingereza, Joe Hart huenda akaondoka Manchester City mwishoni mwa msimu atakapokuwa amemaliza mkataba wa mwaka mmoja kuitumikia Torino ya Italia.
Kocha wa Manchester City, Pep Guardiola amekataa kuzungumzia hatma ya mchezaji huyo hadi mwishoni mwa msimu.
Guardiola hajavutiwa na Joe Hart tangu ajiunge na Manchester City na aliamua kumsajili Claudio Bravo kutoka FC Barcelona na kumtoa Hart kwa mkopo kwenda klabu ya Torino inayoshiriki Serie A.
Hata hivyo Bravo(33) ameshindwa kufanya kile kilichotarajiwa na Guardiola hivyo siku za karibuni amejikuta akimtumia zaidi Willy Caballero aliyetarajiwa kuwa msaidizi wake.
Mkataba wa Caballero(35) unaisha mwishoni mwa msimu lakini Manchester City bado haijafanya nae mazungumzo hivyo kuashiria kuwa huenda klabu hiyo ina mpango wa kusaka mlinda mlango mwingine.
Sambamba na Caballero, Yaya Toure na Bacary Sagna nao mikataba yao inakamilika mwishoni mwa msimu na hakuna mazungumzo ya kuwaongeza mikataba mipya.
Wote wameambiwa wasubiri mpaka mwishoni mwa msimu.
Kocha wa Manchester City, Pep Guardiola amekataa kuzungumzia hatma ya mchezaji huyo hadi mwishoni mwa msimu.
Guardiola hajavutiwa na Joe Hart tangu ajiunge na Manchester City na aliamua kumsajili Claudio Bravo kutoka FC Barcelona na kumtoa Hart kwa mkopo kwenda klabu ya Torino inayoshiriki Serie A.
Hata hivyo Bravo(33) ameshindwa kufanya kile kilichotarajiwa na Guardiola hivyo siku za karibuni amejikuta akimtumia zaidi Willy Caballero aliyetarajiwa kuwa msaidizi wake.
Mkataba wa Caballero(35) unaisha mwishoni mwa msimu lakini Manchester City bado haijafanya nae mazungumzo hivyo kuashiria kuwa huenda klabu hiyo ina mpango wa kusaka mlinda mlango mwingine.
Sambamba na Caballero, Yaya Toure na Bacary Sagna nao mikataba yao inakamilika mwishoni mwa msimu na hakuna mazungumzo ya kuwaongeza mikataba mipya.
Wote wameambiwa wasubiri mpaka mwishoni mwa msimu.
https://play.google.com/store/apps/details?id=com.sn.news&hl=en
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
No comments:
Post a Comment