» » Duh: Tazama Picha Za Gari la Kubeba Kinyesi Likimwaga Maji Machafu Barabarani Maeneo ya Ubungo Leo Asubuhi

ubungo-mavi-7
DAR ES SALAAM: Mapema leo asubuhi, lori la maji taka limechafua hali ya hewa kwenye Barabara ya Morogoro baada ya kumwaga ‘mzigo’ (maji yenye kinyesi) katikati ya barabara hiyo maeneo ya Ubungo Mataa na kusababisha taharuki na harufu kali.



ubungo-mavi-1
Kwa mujibu wa mshuhuda wa tukio hilo, inasemekana kuwa lori hilo lilikuwa likitokea maeneo ya Rombo Kimara ambapo baada ya kufika Ubungo kwenye mataa ya foleni, mfuniko wa tanki uliftyatuka ndipo likaanza kumwaga uchafu huo barabarani. ubungo-mavi-3
Baada ya kuona hali hiyo, dereva wa lori hilo alitoka mbio na kwenda kuziba eneo ambapo uchafu huo ulikuwa ukitoka.ubungo-mavi-4
Hata hivyo watumiaji wa barabara hiyo na wafanyabiashara wa eneo hilo hasa wamachinga wameshangazwa tukio hilo huku wakieleza kuwa ilitakiwa dereva na kondakta wa gari hilo wahakikishe mfuniko wa tanki umekaza kabla ya kuanza safari ili kuzuia ajali kama hizo ambazo zinaweza kuepukika kwa kuzingatia umakini wa kazi.ubungo-mavi-5
Aidha wananchi hao wameitaka Manispaa ya Jiji la Dar  es Salaam imchukulie hatua zinazostahili mmiliki wa gari hilo na dereva wake ikiwa ni pamoja na kumtoza faini au kusafisha barabara kutokana na adha aliyoisababisha ili liwe funzo kwa wamiliki na madereva wengine wa magari ya maji taka.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...