» » Njaa yaweka rehani ubunge wa Zitto

Zitto Kabwe, Kiongozi wa ACT na mbunge wa Kigoma Mjini akihutubia wananchi katika moja ya kampeni zake


Zitto ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini ametoa msimamo wa kujiuzu kupitia ukurasa wake wa mtandao wa Facebook na Twitter.
“Serikali ya CCM ikinionesha tani 1.5 milioni za chakula ambazo inataka kusambaza, najiuzulu Ubunge mara moja. Narudia, mpaka Oktoba 2016 kulikuwa na nafaka tani 90,400 tu kwenye maghala yote ya NFRA.
“Tunashukuru kuwa Hivi sasa ajenda ya tishio la njaa inapata majawabu na matamko. Ndio wajibu wa vyama vya siasa. Kuibua masuala muhimu kwa nchi yetu,” ameandika Zitto.
Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John Magufuli imekuwa ikisisitiza kuwa taifa halijakumbwa na njaa na hakuna chakula cha msaada ambacho serikali itakipeleka kwa wananchi, bali wananchi wafanye kazi kwa bidii ili kujipatia kipato halali.
Hata hivyo, katika baadhi ya maeneo ya nchi, zimeripotiwa taarifa za kuwepo kwa uhaba wa chakula unaotokana na ukame kiasi cha kusababisha vifo vya mifugo kwa kukosa malisho.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...