Rais Mteule wa Marekani, Donald Trump, ametangaza
kuvunjilia mbali shirika lake la utoaji misaada, ili kuzuia aina yoyote
ya muingiliano wa kikazi wakati akiwa Rais. Bwana Trump amesema shirika
hilo limetoa msaada mkubwa wa mamilioni ya dola, ili kufadhili miradi
mbalimbali, lakini sasa ameachana nalo kwa manufaa ya cheo chake mpya
kama Rais wa Marekani. Mwanasheria mkuu wa New York, amekuwa
akichunguza wakfu huo wa kibinafsi wa Bwana Trump, ikiwa unafuata kila
kanuni ya sheria zinazolinda mashirika ya misaada na mchango kwa makundi
mbalimbali ya kisiasa, na mwezi Oktoba mwaka huu, aliamuru ikome
kukusanya fedha.
Pakua App Yetu-Bofya Hapa
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
Share !
Topics:
About 4sn News
Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
No comments:
Post a Comment