» »Unlabelled » Wamarekani waandamana kupinga mauaji ya mtu mweusi

Wamarekani waandamana kupinga mauaji ya mtu mweusi

o
Waandamanaji MarekaniImage copyrightGETTY IMAGES
Image captionMaandamano Marekani
Maandamano yamezuka kwa siku wa pili mfululizo katika mji wa Charlotte, Marekani, kufuatia kifo cha mtu mmoja mweusi aliyepigwa risasi na polisi, Jumanne usiku.
Polisi wa kuzuia ghasia wametumia mabomu ya machozi kutawanya umati mkubwa wa watu wenye hasira waliokuwa wamekusanyika katikati ya mji.
Katika ghasia hizo mtu mmoja aliuawa kwa risasi.
Serikali katika eneo hilo imeyaita mauaji hayo kama ya raia kwa raia.
Maandamano na Ghasia zilizuka Jumanne usiku baada ya polisi kumuua Keith Lamont Scott, huku wakisema kwamba kijana huyo alikuwa na bunduki na kwamba alipuuza wito wa kuweka silaha chini.
Hata hivyo familia ya kijana huyo imesema kuwa hakuwa amebeba silaha yoyote
Meya wa mji huo, Jennifer Roberts, ameiambia BBC kuwa aliwataka polisi kumwonyesha mkanda wa video ya tukio hilo.

ASANTE KWA KUTEMBELEA BLOG YETU WATARIFU NA WENZAKO PIA TUPIA MAONI YAKO

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About IVST TANZANIA

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles