» »Unlabelled » CHADEMA yaahirisha "Oparesheni UKUTA

CHADEMA yaahirisha "Oparesheni UKUTA"

WEDNESDAY , 31ST AUG , 2016

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimetangaza kuahirisha mikutano na maandamano yake (UKUTA) ili kutoa nafasi kwa viongozi wa dini, serikali, vyombo vya dola na wadau kujadiliana kufikia muafaka.

Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe


Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe ametangaza rasmi , kusitisha maandamano na mikutano ya siasa iliyokuwa ifanyike nchi nzima kuanzia kesho Septemba Mosi ili , kupisha nafasi ya viongozi wa dini kukutana na Rais Dkt. John Magufuli kutafuta suluhu ya kisiasa.

Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es salaam Mbowe amesema CHADEMA imefikia uamuzi huo muhimu baada ya vikao na wito kutoka kwa viongozi wa dini wa madhehebu mbalimbali pamoja na asasi za kiraia.

“Viongozi wa dini na asasi za kiraia wametuomba, tusitishe maandamano hayo ili wapate nafasi ya wiki tatu mwezi huu kukutana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli ili kutafuta suluhu ya kisiasa na kama ikishindikana Oktoba Mosi maandamano hayo yataratibiwa upya” amesema Mbowe

Mbowe amesema sababu nyingine ni kuwasubiri wenzao kutoka chama cha wananchi CUF, ambao bado wanakabiliwa na michakato ya uchaguzi ndani ya chama chao, ili waungane na kuwa nguvu moja.

Amelaani vitendo vya kukamatwa kwa viongozi wa chama hicho akiwemo Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho kwa upande wa Zanzibar, Salum Mwalimu, ambapo amesema hadi leo, inakadiriwa wanachama na viongozi wa CHADEMA zaidi ya 230 wamekamatwa na kufunguliwa mashitaka ya uchochezi.

Aidha Mbowe amewataka wana Chadema na wafuasi wa chama hicho kuwa watulivu wakati wakisubiri viongozi wa dini kufanya mazungumzo hayo ili haki yao ya kikatiba iweze kupatikana.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...