» » JIBU MASWALI 50 YAFUATAYO ILI KUJIPIMA UELEWA WAKO WA MAANDIKO

Nakutakia mtihani mwema. 
MIMI NI NANI? 
*Maelezo

Jibu maswali yote 50.

1. Nilikuwa wa kwanza kupanda shamba la mizabubu. Mimi ni nani?
a) Adam
b) Nuhu
c) Kaini

2. Mimi ni mji ambao Paulo alikuta madhabahu yaliyoandikwa kwa “Mungu asiye julikana”. Mimi ni nani?
a) Rumi
b) Galatia
c) Athene

3. Nilikata upindo wa nguo ya Sauli. Mimi ni nani?
a) Daudi
b) Jonathani
c) Samweli

4. Mtume Paulo alitutoa mimi na Iskanda kwa shetani ili shetani atufundishe. Mimi ni nani?
a) Anania
b) Himenayo
c) Baraba

5. Kwangu Mungu alinipulizia pumzi ya uhai. Mimi ni nani?
a) Masikio
b) Pua
c) Roho

6. Mimi ni amri ya kumi. Mimi ni nani?
a) Usitamani
b) Usiibe
c) Usizini

7. Nilisema “mpatie kaisari vilivyo vyake Kaisari na mpatie Mungu vilivyo vyake Mungu”. Mimi ni nani?
a) Mtume Paulo
b) Yesu Kristo
c) Petro

8. Siku Yesu alipoizidisha mikate na samaki watu wakala wakasaza aliniuliza “tununue wapi mikate ili hawa wapate kula?”. Mimi ni nani?
a) Yohana
b) Andrea
c) Philipo

9. Mimi ni mahali ambapo Sarah alifia. Mimi ni nani?
a) Merabu
b) Kaanani
c) Kiriath-arba

10. Nilikuwa mtoto wa mwana wa mfalme lakini nilijichukulia kama mbwa mfu, lakini niliitwa tena na mfalme daudi nikala naye chakula mezani pake. Mimi ni nani?
a) Absalom
b) Mefiboshethi
c) Ahithopheli

11. Nilipofuka nilipokuwa nikienda Damasca. Mimi ni nani?
a) Petro
b) Timotheo
c) Paulo

12. Mimi ni kaka yake Isaka. Mimi ni nani?
a) Esau
b) Ishimael
c) Yakobo

13. Ni kitabu kitakatifu ndani yangu yamo mafundisho juu ya kuutawala ulimi. Mimi ni nani?
a) Waebrania
b) Luka
c) Yakobo

14. Shem, Hamu na mimi ni watoto wa Nuhu. Mimi ni nani?
a) Yafethi
b) Mesharck
C) Jafeti

15. Mimi ni baba yake Raheli. Mimi ni nani?
a) Isaka
b) Manoha
c) Laban

16. Ni kitabu kitakatifu ndani yangu pameandikwa “kila jambo kuna majira yake, na wakati wa kila kusudi chini ya mbingu”. Mimi ni nani?
a) Mhubiri
b) Methali
c) Zaburi

17. Ni kitabu kitakatifu. Ndani yangu yameandikwa maneno: “Mungu ni Roho, na wote wamuabuduo wapaswa kumuabudu katika roho na kweli”. Mimi ni nani?
a) Luka
b) 1 petro
c) Yohana

18. Ni baba yake mfalme  Yothamu, mfalme wa Yuda. Mimi ni nani?
a) Ahazi
b) Hezekia
c) Uzia

19. Kwa mujibu wa kitabu cha methali, Yule atakaye niche/fear atakuwa hai. Mimi ni nani?
a) Dhambi
b) Uovu
c) Bwana

20. Ni kitabu kitakatifu. Ndani yangu yameandikwa maneno: “na kama vile watu wanawekewa kufa mara moja na baada ya kifo hukumu”. Mimi ni nani?
a) Waebrania
b) Waefeso
c) Wagalatia

21. Kaini aliniua. Mimi ni nani?
a) Shemu
b) Abneri
c) Habili

22. Ni kitabu kitakatifu, maneno yangu yanasema moyo uliochangamka ni dawa nzuri. Mimi ni nani?
a) Methali
b) Wimbo ulio bora
c) Zaburi

23. Mimi ni kitabu katika sura yangu ya kwanza ukoo wa Yesu umetajwa. Mimi ni nani?
a) Luka
b) Marko
c) Mathayo

24. Ni mmoja wa wafalme ambao walikosa usingizi. Mimi ni nani?
a) Nebukadneza
b) Yeroboam
c) Ela

25. Mimi ni mwanamke wa kwanza niliyempokea Kristo kwa sababu ya mtume Paulo. Mimi ni nani?
a) Persisi
b) Tryphaena
c) Lidia

26. Baada ya kukutana na mtu Fulani moyo wangu ulibadilika na nikaamua kurudiha vitu vyote nilivyowiwa. Mimi ni nani?
a) Luka
b) Daudi
c) Zakayo

27. Mfalme wa babeli. Mimi ni nani?
a) Nebukadneza
b) Yeoakimu
b) Dario

28. Nilikuwa ni miongoni mwa miji minne iliyotajwa katika Biblia iliyoharibiwa kwa sababu ya hasira ya Mungu. Mimi ni nani?
a) Seboimu
b) Filipi
c) Damasca

29. Nilisema Yesu ataitwa Immanuel (Mungu pamoja nasi). Mimi ni nani?
a) Luka
b) Mathayo
c) Marko

30. Mimi ndiye niliyeanza kuandika kitabu cha Yeremia. Mimi ni nani?
a) Baruku
b) Neri
c) Yeremia

31. Yakobo alinizika betheli. Nilikuwa mlezi wa rebeka. Mimi ni nani?
a) Leah
b) Debora
c) Zilipa

32.  Ni kamanda wa jeshi la Sauli. Mimi ni nani?
a) Abneri
b) Ahinoamu 
c) Naamani

33. Nilimpa Adamu tunda lililokatazwa. Mimi ni nani?
a) Hawa
b) Kaini
c) Nyoka

34. Ni kitabu kitakatifu. Ndani yangu pameandikwa askari 185000 walikufa kwa usiku mmoja. Mimi ni nani?
a) Waamuzi
b) 2 wafalme
c) 1 samweli

35. Ni kitabu kitakatifu. Ndani yangu yameandikwa maneno: “kesheni basi kwa maana hamjui ni siku ipi atakayokuja Bwana wenu”. Mimi ni nani?
a) Luka
b) Mathayo
c) Matendo ya mitume

36. Ni kitabu kitakatifu. Ndani yangu yameandikwa maneno: “kwa jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa mwana wake pekee ili kila mtu amwaminiye asipotee bali awe na uzima wa milele”. Mimi ni nani?
a) Mathayo
b) Luka 
c) Yohana

37. Nilisema “kama tukiishi au kama tukifa, tu mali ya Bwana”. Mimi ni nani?
a) Yohana
b) Petro
c) Paulo

38. Nilimuoa dada yangu (binti wa baba yangu ila sio wa mama yangu). Mimi ni nani?
a) Lutu
b) Ibrahim
c) Labani

39. Mimi ni pango. Ndani yangu Daudi alijificha alipokuwa anamkimbia Sauli. Mimi ni nani?
a) Megido
b) Merare
c) Adulamu

40. Mimi ni mkate ambao Mungu aliushusha kutoka mbinguni ambao ulikuwa mweupe kama chembe za mtama na tamu yake kama maandazi yaliyotengenezwa kwa asali. Mimi ni nani?
a) Matzo
b) Pita
c) Manna

41.  Ni mmoja wa mitume, nilichukua nafasi ya Yuda msaliti. Mimi ni nani?
a) Barnaba
b) Simion
c) Mathiya

42.  Kila siku niliomba na kutoa sadaka kwa ajili ya kuwatakasa watoto wangu. Mimi ni nani?
a) Stefano
b) Ibrahim
c) Ayubu

43. Zaidi ya watu 40 waliapa  kutokula wala kunywa hadi watakapo niua. Mimi ni nani?
a) Paulo
b) Yakobo
c) Petro

44.  Mimi ni baba yake mfalme Ahabu. Mimi ni nani?
a) Omri
b) Zimri
c) Tibini

45.  Mazungumzo kati yangu na mwenzangu tukiwa njiani kuelekea Emau wakati Yesu amefufuka, yalikuwa ni ya kuvutia sana, japo katika agano jipya ni jina langu tu ndiyo lililotajwa. Mimi ni nani?
a) Kleopa
b) Petro
c) Dema

46. Ni mmoja wa wakamwana (daughter-in-law)  wa Naomi. Mimi ni nani?
a) Rebeka
b) Raheli
c) Orpa 

47. Nilikuwa ni mchungaji nilikutana na mme wangu mtarajiwa nilipoenda kunywesha kondoo maji kisimani. Mimi ni nani?
a) Rebeka
b) Ruthi
c) Raheli

48. Nilitupwa kupitia dirishani kwa amri ya kapteni na mwili wangu uliliwa na mbwa. Mimi ni nani?
a) Yezebeli
b) Rahabu
c) Bathsheba

49. Mimi ni mtoto wa kwanza wa Nahori (ndugu yake Ibrahimu). Mimi ni nani?
a) Usi
b) Buzi
c) Hazo

50.  Mimi ni baba yake Yohana mbatizaji. Mimi ni nani?
a) Zakaria
b) Manoa
c) Malaki.

*Nikutakie mtihani mwema*🙋‍♂🙋‍♂🙋‍♂
By Ev Emmanuel Jeremiah

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...