Mkutano mkubwa wa Chama cha Wanataaluma wajasiriamali
wa Kanisa la Wadventista Wasabato Tanzania (ATAPE), umeanza rasmi leo mkoani
Simiyu.
wa Kanisa la Wadventista Wasabato Tanzania (ATAPE), umeanza rasmi leo mkoani
Simiyu.
Pamoja na mambo mengine, mkutano huo umebainisha
mafanikio yaliyofikiwa na chama hicho ikiwamo kupata zaidi ya Sh bilioni moja
katika miradi ya maendeleo nchini.
mafanikio yaliyofikiwa na chama hicho ikiwamo kupata zaidi ya Sh bilioni moja
katika miradi ya maendeleo nchini.
Mkutano huo unaofanyikia katika Shule ya Sekondari
Kusekwa iliyoko Mjini Bariadi, zaidi ya wanataaluma na wajasiriamali 1,500
kutoka maeneo mbalimbali ya nchi wameshiriki.
Kusekwa iliyoko Mjini Bariadi, zaidi ya wanataaluma na wajasiriamali 1,500
kutoka maeneo mbalimbali ya nchi wameshiriki.
Akizungumza na waandishi wa habari Mwenyekiti wa
chama hicho, Freddie Maneto amesema ATAPE kimewekeza katika miradi ya Afya,
Kilimo, Elimu, Maji, pamoja na ujasiriamali.
chama hicho, Freddie Maneto amesema ATAPE kimewekeza katika miradi ya Afya,
Kilimo, Elimu, Maji, pamoja na ujasiriamali.
“Tuna hospitali mbalimbali, shule, mashamba
zaidi ya hekari 10,000 ambayo tumelima mihogo, miti na korosho, hivyo tunapoadhimisha
miaka 20 ya uwepo wa chama chetu, tunajivunia kuwa miongoni mwa taasisi ambayo
imeajiri Watanzania wengi,” amesema Maneto.
zaidi ya hekari 10,000 ambayo tumelima mihogo, miti na korosho, hivyo tunapoadhimisha
miaka 20 ya uwepo wa chama chetu, tunajivunia kuwa miongoni mwa taasisi ambayo
imeajiri Watanzania wengi,” amesema Maneto.
Aidha, mwenyekiti huyo amesema katika kutoa
huduma kwa wananchi, wanatarajia kuleta mradi wa maji mkoani Simiyu, kutokana
na mkoa huo kuwa na changamoto ya upatikanaji wa huduma hiyo kwa wananchi wake.
huduma kwa wananchi, wanatarajia kuleta mradi wa maji mkoani Simiyu, kutokana
na mkoa huo kuwa na changamoto ya upatikanaji wa huduma hiyo kwa wananchi wake.
Hata hivyo, wananchi wa mkoani Simiyu
wameushukuru uongozi wa mkoa kwa kuendelea kuwaletea fursa mbalimbali ambapo
wanategemea kuongeza kipato kupitia biashara zao.
wameushukuru uongozi wa mkoa kwa kuendelea kuwaletea fursa mbalimbali ambapo
wanategemea kuongeza kipato kupitia biashara zao.
“Hii ni fursa kubwa kwetu, kama wananchi wa
Simiyu, watu zaidi ya 15,000 ni wengi tutaongeza kipato kupitia biashara
mbalimbali, kwa sasa katika mji wetu wa Bariadi nyumba za kulala wageni zote
zimejaa, watu wamefanya biashara,” amesema John Bubinza mkazi wa Bariadi.
Simiyu, watu zaidi ya 15,000 ni wengi tutaongeza kipato kupitia biashara
mbalimbali, kwa sasa katika mji wetu wa Bariadi nyumba za kulala wageni zote
zimejaa, watu wamefanya biashara,” amesema John Bubinza mkazi wa Bariadi.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
No comments:
Post a Comment