» » Kigwangallah: Siku za kampuni ya OBC inayomilikiwa na Falme za Kiarabu Loliondo Zinahesabika

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamis Kigwangalla amesema siku za kampuni ya Ortello Business Cooperation (OBC) inayomilikiwa na Falme za Kiarabu kuendelea kuwapo katika Pori Tengefu la Loliondo wilayani Ngorongoro zinahesabika.

Akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Ololosokwani, Dk Kigwangalla alisema mgogoro wa Loliondo uliodumu kwa zaidi ya miaka 26 sasa utapatiwa suluhu na Serikali. 

“Naomba wananchi muwe watulivu Serikali yenu inafanyia kazi matatizo ya Loliondo na kuhusu kampuni ya OBC kama ambavyo nilitaka leseni ya umiliki wa kitalu hiki ikimalizika mwezi Januari hatutawapa nyingine,” alisema.

Alisema kuna sababu nyingi za kutotoa leseni kwa kampuni hiyo ikiwamo kukiukwa kwa sheria ya vitalu ambayo hairuhusu kutolewa leseni katika eneo lenye mgogoro na pia ina eneo kubwa la kilomita za mraba 4,500 ambalo hawalitumii lote kutokana na kuwapo kwa makazi ya watu.

Akizungumza katika kikao hicho, mmoja wa wananchi wa Kijiji cha Ololosokwani ambacho kinapakana na kitalu cha OBC, Koya Timan alisema kampuni hiyo ambayo inapakana na Hifadhi ya Serengeti imekuwa ikiwazuia wafugaji kupata malisho na maji.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn news

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...