» » Zitto anena nyumba yake kuteketea moto

Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe amewataka wananchi kuwa watulivu wakati Jeshi la Polisi likiendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha moto ulioteketeza nyumba yake.

Nyumba hiyo iliteketea jana Jumamosi alasiri na hakuna madhara kwa binadamu yaliyotokea isipokuwa mali zote zilizokuwamo ndani zimeteketea.

“Tumepata ajali kidogo. Nyumba yangu ninayoishi katika eneo la Kibingo, mji mdogo wa Mwandiga, Kigoma imeteketea kwa moto jioni hii. Alhamdulillah, kuwa hakuna binaadam aliyeumia,” aliandika Zitto katika ukurasa wake wa Facebook.

Alisema analishukuru Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, majirani zake na wananchi wenzake kwa ushirikiano walioutoa ili kuzima moto huo.

“Kwa sasa Jeshi la Polisi wanafanyia kazi kujua chanzo cha ajali. Naomba wananchi wawe watulivu wakati Polisi wanaendelea na uchunguzi husika,” alisema Zitto.

Nyumba hiyo aliyoijenga wakati akigombea ubunge kwa mara ya kwanza iko kiwanja kimoja na nyumba yake ya sasa.

Msaidizi wa mbunge huyo, Nyembo Mustafa alisema Zitto hakuwa anaishi kwenye nyumba hiyo baada ya kujenga nyingine kubwa kwenye kiwanja hicho.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...