» » Tume Ya Uchaguzi Kenya Yatangaza Tarehe ya Uchaguzi wa Rais

Tume huru ya uchaguzi nchini Kenya IEBC imetangaza rasmi tarehe ya uchaguzi wa urais, ambao utakuwa wa marudio baada ya Mahakama kuufuta wa awali

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na tume hiyo kwa vyombo vya habari kupitia mitandao ya kijamii ukiwemo wa twitter, IEBC imesema Oktoba 17 ndiyo tarehe rasmi ya kufanyika uchaguzi huo.

"Uchaguzi mpya utafanyika Oktoba 17 mwaka 2017, kufuatia uamuzi wa Mahakama ya Juu wa kufuta uchaguzi wa urais uliofanyika Agosti 8, 2017, hakutakuwa na wagombea wapya, wagombea ni Raila Odinga na mwenzake Kalonzo Musyoka, pia Uhuru Kenyatta na mwenzake William Ruto", iliandika taarifa hiyo.

Uchaguzi huo ulitakiwa kufanyika ndani ya siku 60 tangu uamuzi wa Mahakama ya juu wa kuufuta ule wa awali kutolewa, Septemba 1 mwaka huu.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn news

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...