» » Marekani kuipiga Korea Kaskazini ikimgusa mshirika wake


Trump amesema Korea Kaskazini inajitafutia matatizo


Image captionTrump amesema Korea Kaskazini inajitafutia matatizo
Waziri wa masuala ya ulinzi wa marekani James Mattis amesema kuwa tishio lolote kutoka korea kaskazini kwa Marekani ama washirika wake litajibiwa vikali na jeshi.
Mattis amezungumza hayo baada ya mkutano wake na Rais Trump juu ya masuala ya usalama wa nchi kufuatia jaribio la nyuklia huko Pyongyang.
Trump ameonya kuwa Marekani inaweza kusimamisha kufanya biashara na nchi yoyote inayoshiriki biashara na Korea Kaskazini.
China ndio mshirika mkuu wa baishara na Pyongyang, ameongeza kuwa korea kaskazini imekua tishio na imeleta fedheha kwa Beijing.
Alivyoulizwa na waandishi wa habari kama Marekani itashambuliwa na korea kaskazini, rais trump alisema kuwa tutaona''
Nayo korea kusini imesema kuwa imefanya majaribio matano kama majibu ya jaribio la nyuklia la korea kaskazini.
Rais wa Korea Kaskazini Kim Jong-un, (katikati) akipokea maelekezo ya namna bomu hilo linavyofanya kazi
Image captionRais wa Korea Kaskazini Kim Jong-un, (katikati) akipokea maelekezo ya namna bomu hilo linavyofanya kazi
Rais wa Urusi na Raisi wa china wote wamesisitiza juu ya umuhimu wa kuondokana mzozo wa Korea.
Nao Japan wamesema kuwa jaribio hilo si la kusamehewa.
Jaribio hilo ni la sita kufanywa na kore kaskazini katika kipindi cha miaka 10.
Limesababisha tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 6.3 lilifika katika mkoa wa china uliokaribu na Korea Kaskazini.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn news

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...