» » Barabara aliyopita Rais JPM Kagera, Malori yazidi Kukwama. nisehemu muhimu sana inayo hitaji ukarabati


Eneo la Nyabugombe,wilayani Biharamulo mkoani Kagera Zaidi ya magari 500 yamekwama tangu usiku wa Jana August 4, 2017 katika barabara  kuu ya lami itokayo Nyakanazi –Lusahanga-Rusumo eneo la kijiji cha Nyabugombe kata ya Nyakahura wilayani Biharamulo,mkoani Kagera  kilomita mbili kuingia wilayani Ngara mkoani humo kutokana na barabara hiyo kuharibika tangu ijengwe miaka 32 iliyopita.
Barabara hiyo imeanza kuchimbika na lami kubanduka na kubaki vumbi licha ya kufanyiwa ukarabati wakati wote wa kila mwaka.

Ubovu wake ni kujaa mashimo yanayochangia magari yenye mizigo kushindwa kuendelea na safari, huku mengine yakipinduka baada ya kupanda milima na hata kurudi nyuma.



Wakizungumza na Mwandishi wa Mtandao huu  katika eneo hilo, baadhi ya  madereva wamesema eneo hilo ni bovu miaka yote na unapofanyika ukarabati, wakandarasi wanatumia saruji rojorojo bila kuzingatia kuwa magari yanayopita yanakuwa na tani nyingi za mizigo.

Wamesema  magari  hayo yanasafiri kutoka  na kuingia Dar Es Salaam hadi  Rwanda na Burundi na hata Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo DRC,  kwa kuingiza  fedha zinazoweza  kuinua uchumi wa Taifa,  hivyo serikali ya Tanzania  haina budi kujenga upya barabara hiyo, kutoka Nyakanazi wilayani Biharamulo hadi Rusumo   Wilayani ya Ngara mkoani Kagera.


Kukwama kila wakati kwa magari katika eneo hilo la Nyabugombe , safari za magari ya abiria kutoka Ngara kwenda mikoani kupitia eneo la barabara hiyo zimekuwa zikisimama kwa saa kadhaa huku huduma za kijamii kama maji,  mighahawa ya kuuzia chakula , zahanati na mawasiliano ya mitandao ya simu za mkononi vikikosekana na kuleta changamoto kwa wasafiri.

Hata hivyo Mhandisi wa barabara wa mkoa wa Kagera Bw.Chakindo Nasiri, alipotafutwa kwa njia ya simu amesema barabara hiyo inahitaji kujengwa upya, na kinachofanyika hivi sasa ni ukarabati mdogo ili kuwezesha magari kupita kusafirisha bidhaa kuelekea nchi za Rwanda. Burundi na DRC.


Picha Na Shaban Ndyamukama.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn news

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...