Haki miliki ya pichaAFPImage captionVitisho vya China vyasababisha Vietnam kusitisha uchimbaji wa gesi
Vietnam imesitisha shughuli ya uchimbaji gesi katika eneo linalozozaniwa kusini mwa bahari ya China, kufuatia vitisho vikali kutoka China.
Taarifa zinaiambia BBC kuwa kampuni iliyokuwa ikiendesha uchimbaji huo iliamrishwa kuondoka eneo hilo.
Inajiri siku chache baada ya kampuni ya Respol kusema kuwa imegundua gesi nyingi.
China yazindua manowari mpya ya kijeshi
Ripoti zinasema kuwa wakurugenzi wa Respol waliambiwa wiki iliyopita na serikali wa Viertman kuwa China ilikuwa imetisha kushambulia vituo vyake katika visiwa vya Spratly ikiwa uchimbaji huo haungesitishwa.
Image captionVitisho vya China vyasababisha Vietnam kusitisha uchimbaji wa gesi
China inadai kuwa karibu eneo lote la kusini mwa bahari ya China ni lake, visiwa ambavyo pia vinavyodaiwa na mataifa mengine.
China: Hatua ya meli ya Marekani kukaribia kisiwa ni uchokozi mbaya
Vietnam inaliita eneo hilo Block 136-03 na imeipa zabuni kampuni inayoitwa Talisman-Vietnam.
China nayo inaliita eneo hilo Wanan Bei-21 ikiwa imetoa kandarasi kwa kampuni tofauti.
Haki miliki ya pichaAFPImage captionVitisho vya China vyasababisha Vietnam kusitisha uchimbaji wa gesi
No comments:
Post a Comment