» » THE CIVIC UNITED FRONT. JUMUIYA YA VIJANA CUF. IDARA YA VYUO VIKUU.


Leo tarehe 23/8/2017 baadhi vijana wa JUVICUF chini ya kamati ya vyuo vikui walifika nyumbani  kwa lengo la kumjuilia hali mzee wetu, MACHANO KHAMIS na kubadilishana naye mawazo.

Mzee machano ni miongoni mwa waasisi wa CHAMA CHA WANANCHI-CUF ambae kwa sasa anasumbuliwa na maradhi ya uzeeni. Huenda wengi wa vijana hata hawamfahamu mzee huyu.

Miongoni mwa aliotusimulia na kutueleza kwa kina ni historia ya mapambano ya kutafuta haki kwa kila Mtanzania.

Akisimulia wakati walipofukuzwa kutoka katika CCM alisema.
"...kabla hatujafukuzwa, akina Salim Ahmed Salim walimwambia Nyerere, ukiwafukuza hawa CCM utakuwa kushaiuwa Zanzibar. Na ni kweli CCM tulizika kabisa."

Tulimuliza kama lau akipewa nafasi ya kupendekeza ni nani awe mrithi Maalim alisema. "NI NYINYI VIJANA. Sisi shida yetu ni mtu yeyote atakaekuwa tayari kupigania maslahi ya wananchi wa Zanzibar na Bara. Kila mtu apate haki yake kwa usawa kabisa"

Alipoulizwa ni wasifu gani haswa anaojipambanua Maalim Seif anaoufahamu. Mzee machano alisema.
*Maalim ana tabia moja.*
*Hana unafiki moyoni mwake.*
*Haongopi katika maneno yake.*
*Haanguki katika mipango yake.*
*Akikuahidi basi atatekeleza*

Na alipoulizwa kama ni lini alikutana na Maalim. Alisema kuwa ni hivi karibuni tu. Maalim huwa anakuja hapa na kunisalimia. Na hajawahi kunitupa hata kidogo.

Kuhusu suala la ukombozi wa Zanzibar alisema.
*Zanzibar itakomboka leo hii kabla ya kesho. Hatuwezi kuelekea 2020 kama Zanzibar haipo mikononi kwetu. Maalim atakuwa Rais kabla ya 2020. Nina hakika na matumaini makubwa*

Tulikuwa na mengi sana tuliojifunza. Ila kubwa ni maneno yake ya busara kwetu vijana.

*Nakuhusieni kutokuyumbishwa. Nendeni mkawakomboe vijana wenzenu waliofungwa mawazo. Na PENDENI NCHI YENU KWANZA KISHA NDIO MUJIPENDE WENYEWE*

Namuombea kwa Allah ampe afya njema ili awe nasi siku ya jua jipya kichomoza. Ampe hatima njema pale atapomuhitaji mja wake.

MOH'D RAJAB.
Mkuu wa idara ya vyuo vikuu,
JUVI-CUF TAIFA.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Magazeti ya Leo Jumatatu ya July 24
»
Previous
KAMA VIJANA TUNGETAMBUA MAANA HARISI YA NENO NAKUPENDA

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...