» » Rais Magufuli Aagiza milioni 200 za mradi wa maji jeshini zitumike kwa wananchi


Rais John Magufuli ameagiza Sh200 milioni zilizopangwa kutumika katika mradi wa maji katika kambi ya jeshi zianze kuimarisha miradi ya maji kwa  wananchi kwanza.

Akizungumza leo, Alhamisi Julai 20  katika ziara  yake akiwa ameambatana na Rais wa Burundi, Pierre Nkurunzinza, Magufuli amesema  amebaini kuwa pampu za maji wilayani Ngara zimeharibika kwa zaidi ya wiki tatu na kuwa wilaya hiyo ina uhaba mkubwa wa maji.

 Alimuita, Mhandisi wa Maji ajieleze ni kwa nini pampu hizo hazifanyi kazi na baada ya kumsikiliza ndipo alipofanya uamuzi huo.

Akifafanua kuhusu hali ya maji, mhandisi huyo amesema awali visima vya maji wilayani hapo vilikuwa vikihudumia watu 400 lakini kwa sasa wilaya hiyo ina watu zaidi ya 240,000 na hivyo visima hivyo havitoshelezi.

“Tulikuwa tuna idadi ndogo ya watu sasa hivi imeongezeka, lakini tangu pampu iharibike, tumetengeneza mbili na kisima kimoja hakina pampu,” amesema.

 Baada ya mhandisi huyo kufafanua hayo ndipo Rais alimuita Mkurugenzi wa Halmashauri kueleza mipango yake, ndipo Mkurugenzi huyo aliposema mradi wa maji wa Sh200 milioni utaanza kwanza katika kambi ya jeshi.

Kauli hiyo ndiyo iliyomfanya Rais Magufuli kushauri fedha hizo zitumike katika miradi ya maji katika makazi ya wananchi kwanza.

“Wanajeshi wapo 200 na wananchi wapo zaidi ya 20,000 sasa si bora waanze wananchi kwanza,” amesema.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...