» » Prof. Lipumba awavua uanachama wabunge 8 wa CUF pamoja na Madiwani Wawili


Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la Chama cha Wananchi (CUF) limewavua uanachama wabunge wanane wa chama hicho kwa madai ya utovu wa nidhamu ikiwa ni pamoja na kukisaliti chama hicho.

Akizungumza jana na waandishi wa habari katika ofisi za Makao Makuu ya CUF, Buguruni jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba alisema, mbali na wabunge hao, baraza hilo pia limewavua uanachama madiwani wawili wa viti maalumu wa Mkoa wa Dar es Salaam, kwa makosa kama hayo.

Lipumba amesema wabunge hao waliovuliwa uanachama ni miongoni mwa wabunge kumi waliosusia wito wa kwenda kujieleza juu ya tuhuma zinazowakabili za kula njama na CHADEMA ili kuweza kumuondoa yeye madarakani.

Aidha, Lipumba aliwaambia waandishi wa habari kuwa, taarifa kuhusu uamuzi huo tayari zimeshatumwa kwenda kwenye Ofisi ya Spika wa Bunge na Msajili wa Vyama vya Siasa kwa ajili ya hatua zaidi.

Wabunge 10 walioitwa kuhojiwa na chama hicho inadaiwa kuwa ni wale wanaomuunga mkono Katibu Mkuu, Maalim Seif.

Baadhi ya wenyeviti wa serikali za mitaa zilizopo chini ya CUF, wamesema binafsi hawatokuwa tayari kuhojiwa kwani hawamtambui kiongozi huyo.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...