» » Mshindi wa tuzo ya Nobel China, Liu Xiaobo, aaga dunia


Image captionLiu Xiaobo amefariki

Mshindi pekee wa tuzo ya amani ya Nobel nchini China, Liu Xiaobo, amefariki.

Wakati wa kifo chake alikuwa na umri wa mika 61 na ni saa 48 tu zilizopita tangu alipoondolewa gerezani na kukimbizwa hospitalini, ili kutibiwa maradhi ya saratani.

Bwana Liu alikuwa akitumikia kifungo cha miaka 11 jela, kwa kosa la kusambaza shinikizo kwenye mitandao, akitoa wito kwa China kukomesha utawala wa chama kimoja cha kisiasa.

Madaktari watofautiana kuhusu matibabu ya Liu XiaoboChina yamuachilia mshindi wa tuzo ya amani ya Nobel mgonjwa

Mataifa ya magharibi na mashirika ya kutetea haki za kibinadamu kote duniani, yamekuwa yakitoa wito kwa Beijing kumkubalia Bwana Liu Xiaobo kwenda nje ya nchi ili kutibiwa, lakini China ikakataa.

Image captionMshindi wa tuzo ya amani ya Nobel China, marehemu Liu Xiaobo, aonekana akatika picha hii iliyopigwa siku mbili zilizopita akitoka Gerezani

Liu Xiaobo alikuwa mwaandishi na mwanasiasa, msomi mwenye sifa kubwa, ambaye daima alikuwa akishinikiza kuwepo kwa mabadiliko ya amani ya kisiasa.

Alikuwa mmojawepo wa mshirika mkuu wa wanaounga mkono kuwepo kwa maandamano ya demokrasia katika uwanja wa Tiananmen Square mnamo mwaka 1989.

Mshirikishe mwenzako

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...