» » Mishahara ya rais na wabunge yapunguzwa Kenya Hivi ni viunganisho vya nje na vitafungua katika dirisha mpyaSambaza habari hii Facebook Sambaza habari hii TwMshirikish


Tume ya Mishahara KenyaHaki miliki ya pichaSRC
Tume ya mishahara na marupurupu ya watumishi wa umma nchini Kenya imetangaza kupunguzwa kwa mishahara ya maafisa wakuu wakiwemo rais na wabunge.
Mwenyekiti wa tume hiyo Bi Sarah Serem ametoa mpangilio mpya wa malipo ambao anasema utaokoa jumla ya Sh8 bilioni (dola 80 milioni za Marekani) kila mwaka na kupunguza jumla ya mishahara inayolipwa watumishi wa umma kwa asilimia 35 .
Tume hiyo imependekeza kufutiliwa mbali kwa marupurupu ya kipimo cha usafiri wa magari kwa magavana na wabunge na badala yake hilo litakuwa likifidiwa na mfumo mpya wa marupurupu kwa kuzingatia kanda.
Rais sasa atakuwa akilipwa Sh1.4 milioni (dola 14,000) kila mwezi badala ya Sh1.65 milioni (dola 16,500), naye naibu wake awe akilipwa Sh1.2 milioni (dola 12,000).
Mawaziri watakuwa wakilipwa Sh924,000 (dola 9,200), Spika wa Bunge Sh1.1 milioni (dola 11,000) nao magavana wa kaunti Sh924,000 (dola 9,240).
Mabadiliko hayo yataanza kutekelezwa tarehe 8 Agosti, 2017.
Bi Serem amesema maafisa wa serikali walikuwa wakitumia vibaya mfumo wa marupurupu wa kupimiwa usafiri wa magari.
Badala yake, maafisa sasa watakuwa wakilipwa marupurupu ya kila mwezi ya usafiri kwa kutegemea eneo anamotoka afisa husika.
Magavana na manaibu wa magavana pia hawatakuwa wakilipwa tena marupurupu.
Wabunge, ambao wamekuwa wakilipwa marupurupu kwa kuhudhuria vikao vya kamati mbalimbali, pia watakosa marupurupu hayo.
Viongozi wa serikali ya upinzani bungeni, ambao pia walikuwa wakipokea marupurupu ya majukumu maalum pia hawatalipwa tena marupurupu hayo.
Mishahara hiyo mipya itaanza kutekelezwa baada ya uchaguzi mkuu wa Agosti.
Maafisa ambao mihula yao haitakuwa imemalizika mwaka huu wataendelea kupokea mishahara yao ya awali.
Hata hivyo, watakaorithi nyadhifa hiyo watalipwa kwa kufuata utaratibu mpya.

Mishahara mipya:

  • Rais: Sh1.4 milioni kutoka Sh1.65 milioni
  • Naibu Rais: 1.2 milioni kutoka 1. 4 milioni
  • Mawaziri: Sh924,000 kutoka Sh1.056 milioni
  • Makatibu wa Wizara: Sh765,000 kutoka Sh874,000
  • Magavana: Sh924,000 kutoka Sh1.056 milioni
  • Wabunge: Sh621,000 kutoka Sh710,000
  • Maspika: Sh1.155 milioni kutoka Sh1.30 milioni
  • Naibu Spika: Sh924,000 kutoka Sh1.006 milioni
  • Viongozi wa Serikali na Upinzani Bungeni: Sh765,000 kutoka 1.020 milioni
  • Madiwani (Wawakilishi wa Wadi): Sh144,000 kutoka Sh165,000
  • Mawaziri wa Serikali za Kaunti: Sh259, 875 kutoka Sh350,000

Tuma picha/ habari what-sap 0769436440






BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS



tupe maoni yako

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...