» » Mourinho :Sifurahishwi na usajili


Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionJose Mourinho

Meneja wa Manchester United, Jose Mourinho amedaiwa kutofurahishwa na taratibu za usajili zinavyoendelea wa kipindi hiki cha majira ya kiangazi katika klabu yake .

Baada ya United kutwaa taji la michuano ya Europa ligi,meneja huyo alisema alimpa makamu mwenyekiti wa timu hiyo Ed Woodward orodha na wachezaji anaowahitaji kusajili.

Man United haijafanikiwa kusajili wachezaji ambao kocha huyu anawataka katika kujenga kikosi kipya kwa ajili ya msimu ujao.

Kuna uwezekano kukawa na maendeleo mengine wiki hii lakini mpaka sasa ni mchezaji mmoja mpya aliyesajili ambaye ni beki Victor Lindelof toka Benfica ya Ureno.

Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionVictor lindelof

Mourinho anahitaji mshambuliaji mmoja atakayeziba pengo la Zlatan Ibrahimovic, pamoja na kiungo mkabaji.

Man United wamekuwa wakimuwania mshambuliaji wa Real Madrid, Alvaro Morata ambae uhamisho wake bado haujulikani hatima yake.

Lakini pia timu hiyo inawahitaji viungo Eric Dier wa Tottenham na Nemanja Matic kuja kujenga safu bora ya kiungo cha chini .

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...