Rais wa Misri Abdul Fattah al-Sisi, ameidhinisha mkataba ya umiliki wa visiwa viwili vilivyoko katika maeneo ya bahari ya Sham, kwa Saudi Arabia.
Wakili wa serikali Rafiq Sharif, amesema kuwa amri hiyo ya Rais Sisi, imekuwa sheria na kwa sasa visiwa hivyo vitakuwa ni mali ya Saudi Arabia.
Lakini bado mahakama ya kikatiba inafaa kutoa agizo lake la mwisho, ambapo taasisi hiyo ya kisheria na Bunge la nchi hiyo, ndio yaliyo na uwezo wa kutoa agizo la mwisho.

Muafaka huo, umekuwa ukipingwa na kuzuiwa kufanya kazi katika vuta ni kuvute iliyokuwepo, kwa mwaka mzima nchini Misri.
Hatua ya kuachia Saudi Arabia visiwa hivyo, vilisababisha maandamano na pingamizi kubwa kutoka kwa raia nchini Misri, pale agizo hilo lilipotangazwa mwaka jana na Rais al Sisi.
Mwaandishi wa BBC mjini Cairo, anasema kuwa ikiwa Misri haitokubalia kuachia Saudi Arabia visiwa hivyo, bila shaka huenda wakanyimwa fedha nyingi za uwekezaji kutoka kwa taifa hilo la kiarabu, lenye uchumi mkubwa.

Tuma picha/ habari what-sap 0769436440
BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI